THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

INFORMATION AND COMMUNICATION TECHNOLOGIES COMMISSION

Hongereni sana Tume ya TEHAMA

  • News

Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete akikabidhi cheti kwa Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Tehama (ICTC), Dkt. Nkundwe Mwasaga kwa niaba ya watoa mada kuu walioshiriki katika Kongamano la Nne la Kitaaluma la Biashara na Uchumi lililofanyika jana jijini Dodoma chini ya uratibu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE). Dkt. Kikwete aliyekuwa mgeni rasmi katika kongamano hilo, alikabidhi vyeti kwa kutambua mchango wa wazungumzaji hao kwenye tasnia ya Taaluma, Biashara na Uchumi na kipekee, aliishukuru Tume ya Tehama kwa kutekeleza vyema majukumu yake tangu ilipoasisiwa katika Serikali ya Awamu ya Nne. (Mpiga Picha Wetu).