THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

INFORMATION AND COMMUNICATION TECHNOLOGIES COMMISSION

Tume ya Tehama kuendeleza wabunifu nchini

  • News

Arusha, Serikali kupitia Tume ya Tehama imeanza kutekeleza mpango wa kukuza na kuendeleza wabunifu wa Tehama nchini  kwa kuanzisha vituo kila mkoa ili kuwawezesha vijana kupata sehemu maalumu ya kuweza kuendeleza bunifu  zao kwa njia ya Tehama.

Hayo yamesemwa leo Februari  28, 2023  jijini Arusha  Katibu Tawala msaidizi uchumi na mzalishaji Mali mkoa wa Arusha, Daniel Loiruck wakati akizungumza katika mkutano wa wadau wa ubunifu  katika Tehama  uliowashirikisha vijana zaidi ya 150 kutoka mkoani Arusha.

Amesema kuwa, mkutano huo  unalenga kujadili mashauriano na kubadilishana uzoefu katika kuanzisha na kuendesha shughuli za ubunifu kwa kutumia TEHAMA.

Source: Happy Lazaro